Inakuwaje kama tukiondoa moja ya magonjwa kongwe duniani?
1,446,034 views |
Caroline Harper |
TED2018
• April 2018
Trakoma ni ugonjwa wa macho wenye maumivu ambao husababisha upofu. Umekuwepo kwa takribani maelfu ya miaka, na karibuni watu milioni 200 duniani wapo katika hatari ya ugonjwa huu. Kinachoudhi ni kwamba, anasema Caroline Harper, unaweza kutibika kabisa. Akiwa na taarifa za kutosha kutoka mradi wa ramani ya sehemu zenye trakoma, taasisi yake ya Sightsavers wana mpango: kuweka juhudi katika nchi ambazo zina fedha za kuondoa tatizo -- na kuweka mkazo wa juhudi zaidi pia katika nchi ambazo zina mahitaji makubwa. Lengo: kuufanya ugonjwa ubaki kuwa historia katika vitabu tu. Mradi huu imara ni moja ya mawazo ya Audacious Project, mpango mpya wa TED wa kuhamasisha mabadiliko ya kiulimwengu.